YANGA YAKAA KILELENI BAADA YA KUIFUNGA COASTAL UNION 1-0.

2/04/2015 11:24:00 pm
Haroub Cannavaro akishangilia Goli, baada ya kuifungia Yanga dhidi ya Coastal Union

Golikipa wa Coastal Union akiokoa baadhi ya hatari katika lango lake dhidi ya Yanga SC.
TIMU ya YANGA SC imefanikiwa kukaa kileleni mwa ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara baada ya kuifunga Coastal Union ya Tanga kwa 1-0, katika mchezo uliofanyika Mkwakwani Tanga leo.
Kutokana na matokeo haya sasa Yanga imefikisha pointi 22 ikicheza michezo 12, moja zaidi ya mabingwa watetezi AZAM FC wenye pointi 21 katika michezo 11.
Goli la Yanga limefungwa na Haroub Cannavaro katika dakika ya 12 kwa mpira wa kichwa kutokana na mpira wa kurushwa kutoka kwa Mbuyu Twite.

0 comments:

Post a Comment