![]() |
| Ivo Mapunda Kipa wa Simba SC. |
Mchezo huo wa raundi ya nane, ulipigwa jana kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Baada ya mchezo huo, mashabiki walitoa lawama kwa Mapunda kuwa ndiye aliyechangia kufungisha bao hilo kutokana na kutokuwa makini langoni.
Lakini wakati mashabiki wakisema hivyo, kocha wa timu hiyo, Patrick Phiri alitoa lawama zake kwa washambuliaji wake kwa madai kuwa walishindwa kutumia nafasi nyingi walizopata.“Tumefungwa bao la kimichezo sina haja ya kutoa lawama kwa mtu, lakini safu ya ushambuliaji haikuwa makini na imepoteza nafasi nyingi za wazi,” alisema Phiri.

0 comments:
Post a Comment