COUTINHO AINUSURU YANGA , KOMBE LA MAPINDUZI 2015.

1/07/2015 12:46:00 am
Andrey Coutinho  ameifungia bao pekeeYanga SC katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Shaba ya Pemba katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi Kombe la Mapinduzi uliofanyika  Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Coutinho alifunga bao hilo dakika ya 86 kwa mpira wa kichwa akimaliziana krosi ya beki wa kulia, Juma Abdul.
Yanga SC inamaliza ikiwa kinara wa kundi lake baada ya kushinda mechi zake zote tatu za Kundi A, 4-0 mara mbili dhidi ya Taifa Jang’ombe na Polisi na leo 1-0.



0 comments:

Post a Comment