![]() |
| Deogratius Munishi, Kipa Yanga SC. |
Yanga na Azam ziliumana kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa ambapo timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
Bocco ambaye aliingia dakika ya 64 akichukua nafasi ya Salum Aboubakar ‘Sure Boy’, alifanikiwa kufunga bao la kusawazisha dakika ya 65 akiunganisha krosi iliyopigwa na Himid Mao.
Baada ya mchezo huo kumalizika, Pluijm alionekana akimfokea Dida kwenye benchi akimtuhumu hakuwa makini golini na kusababisha hadi Bocco kufunga.

0 comments:
Post a Comment