MTIBWA SUGAR YASHIKWA ASUBUHI:

12/29/2014 02:35:00 pm
Mtibwa Sugar.
TIMU ya Mtibwa Sugar, imebanwa mbavu katika uwanja wake wa nyumbani wa Manungu baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Stand United ya Shinyanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliofanyika asubuhi ya jana.

Mchezo huo ulilazimika kuchezwa tena jana saa 2:00 asubuhi, baada ya kuvunjika juzi katika dakika ya nane kipindi cha kwanza kutokana na mvua kubwa iliyonyesha huku timu hizo zikiwa bado hazijafungana.

Katika mchezo huo uliokuwa na kasi kubwa kwa muda wote, Stand ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao lililofungwa na Shaban Kondo katika dakika ya 22, wakati Said Mkopi iliisawazishia Mtibwa katika dakika ya 86.
Stand United.
Akizungumza na Championi, kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime, alisema mchezo ulikuwa mgumu kwa kuwa kila timu ilikuwa ikisaka pointi tatu muhimu.

“Mechi ilikuwa ngumu kwani wapinzani wetu (Stand United) nao walicheza vizuri,” alisema Maxime.
Naye kocha wa Stand, Mathias Lule, alisema vijana wake walicheza vizuri na anashukuru kupata pointi moja katika mchezo huo wa ugenini.

“Tumecheza vizuri katika kila idara na Mtibwa nao wakiwa nyumbani wamecheza vizuri pia ndiyo mpira ulivyo tunashukuru kuambulia pointi moja,” alisema.

0 comments:

Post a Comment